EAPCO 2023:Askari Polisi wa Rwanda  watwaa vikombe 9

Share Now

Rwanda imekuwa mwenyeji wa mashindano ya  askari polisi kutoka mataifa ya ukanda wa Afrika ya mashariki ‘Eastern Africa Police Chiefs Cooperation Organization (EAPCCO)’. Mashindano haya yalianza  tarehe 21-27 Machi 2023 mjini Kigali.

Mashindano hayo yameandaliwa chini ya kaulimbiu ‘’ Kukuza ushirikiano wa polisi katika kupambana na uhalifu unaovuka mipaka pamoja na ushirikiano wa polisi kupitia michezo na burudani’’.

 
Kamanda mkuu wa Askari Polisi Rwanda  “IGP”, DCG Namuhoranye Felix   akikabidhi kombe mchezaji

Michezo ya EAPCO 2023 imezileta kwa pamoja Uganda,Kenya, Sudani Kusini, Burundi, Ethiopia, Kenya, Sudani na mwenyeji  Rwanda ambayo imepokea kwa mara ya kwanza  Awamu ya nne ya mashaindano hayo.

“EAPCCO Games 2023”, Timu ya Polisi ya Rwanda imemaliza ikiwa  kwenye nafasi a kwanza baada ya kunyakua vikombe  9  kati ya michezo 13 iliyochezwa.

Viongozi wa ngazi mbali mbali za usalama, ulinzi na EAPCCO

Timu zilizoshiriki michezo mbali mbali ikiwemo  soka, Volleyball, riadha, Basketball, Darts, Ndondi, Basketball, Handball, Judo, Karate, Taekwondo, Netball, na kulenga shabaha “Shooting’’. Wachezaji  wote kwa jumla walioshiriki walikuwa 1250 wanaume na wanawake.

Katika mchezo wa soka, timu y Askari Police ya Rwanda ilifunga ya Burundi kwa mikwaju ya penati baada ya timu hizo kuondoka suluhu  kwa magoli 3-3. Mechi ya kwanza Police ya Rwanda iliinyuka Burundi maarufu Rukinzo kwa magoli 3-1 na mechi ya pili Timu ya Polisi Burundi ikaibwaga Rwanda 2-0. Baada ya dakika 120 timu zote zikiwa sare ya 3-3 ilipigwa mikwaju ya penati Rwanda ikaingiza 5-4 Police ya Burundi, kombe likabaki nyumbani Rwanda.

Police Rwanda mabingwa wa Handball baada ya kuikandika Uganda

Kwa jumla Askari Polisi wa Rwanda, walinyaka nafasi ya kwanza, Kenya ni ya pili wakati Uganda ikija kwenye nafasi ya 3.

Timu askari Polisi ya Uganda ilinyakua kombe la Netball iyochezwa na wanawake, Tanzania ilitwaa kombe la Darts wanaume, Kenya ilitwaa kobe la riadha wakati Burundi ilitawazwa kombe la Judo.

Rwanda ilizolea vikombe  vya Basketball, Volleyball, Ndondi, Karate, Kulenga shabaha kwa kutumia bunduki na Pisto, waliibuka pia kombe la soka, Handball.

Mabingwa wa Police Handball Club EAPCCO 2023
Police Burundi wakikabidhiwa kombe na Mkuu wa jiji la Kigali Rubingisa Prudence

Christopher Karenzi


Share Now

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *