APR BBC yatawazwa mabingwa 2025
Timu ya mpira wa kikapu ya APR BBC imetawazwa mabingwa wa ligi kuu ya Rwanda mwaka huu 2025.
Hii ni kufuatia ushindi wa alama 81-72 dhidi ya timu ya Nishati REG baada ya kuinyuka kwa jumla ya mechi 4-1 kwenye fainali iliyomalizika ijumaa tarehe 11 Julai 2025 katika uwanja wa BK Arena jijini Kigali, Rwanda.
Mechi zote kwa jujumla zilikuwa kali pande mbili ila APR ilikuwa makini sana na kuondoka na ushindi wa mechi 4 kwa moja kwenye mechi za fainali (Playoffs).
Hili ni taji la 3 mfululizo kwa APR, itawakiklisha Rwanda mwakani kwenye michuano ya Ligi ya Afrika BAL 2026 itakayofanyika jijini Kigali mwakani.

APR imetwaa mataji 16 ya ubingwa: 1995, 1996, 1997, 1998, 1999, 2000, 2001, 2002, 2003, 2005, 2006, 2008 and 2009 and 2023, 2024 and 2025.

Wachezaji wa APR wakifurahia ushindi.
Kutokana na ushindi huu Timu hii imezawadiwa kombe na kitita cha faranga Milioni 15 za Rwanda.
Miaka 5 iliyopita 2009 timu zilizotwaa taji la ubingwa ni hizi zifuatazo
2025: APR
2024: APR
2023: APR
2022: REG
2021: REG
2020: Patriots
2019: Patriots
2018: Patriots
2017: REG
2016: Patriots
2015: Espoir
2014: Espoir
2013: Espoir
2012: Espoir
2011: Kigali Basketball Club
2010: Kigali Basketball club
2009: APR.
Christopher Karenzi

