Emmanuel Okwi : Hakuna muda wa kulegeza unapocheza soka
Emmanuel Okwi ni mchezaji maarufu wa soka kutoka nchini Uganda akiwa amesajiliwa na Club ya AS Kigali hapa nchini Rwanda. Alicheza katika vilabu mbali mbali barani Afrika na Ulaya . Nimefanya mahojiano naye, nimeanza kumuuliza Okwi ni mtu gani?

Emmanuel Okwi : Kwanza kabisa ni mchezaji anayeogopa Mungu, ni mtu ambaye anajituma siku zote uwanjani, kila nafasi anayopata anahakikisha kwamba anapambana, anaisadia timu yake anayoichezea na vile vile kuungana na wenzake na kufanya kazi kwa pamoja.
Brightafrica.rw: Umecheza katika timu mbali mbali, leo upo katika kikosi cha AS Kigali timu ya jiji la Kigali, mkataba wako na Club ni wa muda gani?
Emmanuel Okwi : AS Kigali, nimesaini mkataba wa mwaka mmoja wakati huu ndo tunaingia wa pili wa ligi kuu msimu huu wa 24/2025, kwa wkati huu bado nina miezi 6 kwenye mkataba wangu.Niko kwa ajili ya kusaidia timu yangu kuhakikisha inamalizia kwenye nafasi nzuri kwenye ligi na kombe la Amani.
Brightafrica.rw: Ulisajiliwa wakati ligi tayari ilianza mapema mwaka jana na wewe ni miongoni mwa wafungaji bora kwenye mzunguko wa Kwanza wa ligi, una siri gani ya kupachika mabao langoni?
Emmanuel Okwi : Ehh unajuwa siku zote ni kuungana na wenzio, ukiwa na wachezaji wazuri , mfano katika timu yetu tuna wachezaji wazuri wanaojituma, wanapambana lakini pia namshukuru Mungu kwasababu sikuwa na pre season nzuri , hata hivo mambo hayajawa mabaya.
Nashukuru Mungu. So… ni hivo kujituma na kuhakikisha ukipata nafasi unaitumia.
Brightafrica.rw: Ligi kuu ya soka ya Rwanda msimu huu wa 2024/25 unaionaje labda tofauti na ligi zilizopita ?
Emmanuel Okwi: Ligi ni ngumu kwa sababu wameongezeka wachezaji wa kigeni, ushindani unakuwa juu zaidi ndo maana timu hazijaachana sana kwa pointi nyingi timu ni kama zinalingana nguvu. Msimu wa 2021/22 nilipokuwa hapa kuna tofauti kidogo, msimu huu ni mgumu sana lakini ni vizuri pia ili kuinua viwango vya wachezaji.
Hakuna muda tena wa kulegeza kuhisi kwamba mambo ni mepesi, lazima ujitume kila siku na uhakikishe unapata nafasi ya kucheza usipojituma ndo hivo utakuwa unakaa nje.
Brightafrica.rw: Mbali na AS Kigali nitajie timu zingine ulizowahi kuchezea.
Emmanuel Okwi: Nilianzia Villa Sports Club katika timu ya watoto (junior) nilipanda hadi timu kubwa ya Villa nchini Uganda, halafu nikasajiwa na Simba SC, baadae Etoile du Sahel ya Tunisia ; sijakaa sana pale kutokana na mambo mbali mbali nikarudi Simba baadae nikaondoka na kuelekea Denmark.
Okwi ameeleza orodha ya timu nyingine huko Uganda, kacheza msimu mmoja baadae akaelekea Yanga, akarudi tena Simba ambako alicheza kwa kipindi kirefu. Alimaliza mkataba wake 2019 katika club hiyo ya Msimbazi.

Baadae alisafiri hadi Misri, alicheza misimu miwili baadae alisajiliwa na Club ya Kiyovu kisha akaelekea nchini Iraq, alovomaliza mkataba huko alirejea nyumbani Uganda halafu baadae alipata usajili wa AS Kigali msimu huu.
Brightafrica.rw: Baada ya safari hiyo ndefu nieleze sasa mafanikio licha ya kwamba bado upo kwenye soka :
Emmanuel Okwi: Mafaniko ambayo naweza kusema zaidi, nimejifunza vitu vingi , nimejifunza tamaduni na mila mbali mbali ukiachana na mapato yaani pesa. Ni vitu nadhani vitanisaidia hata nikimaliza kucheza mpira , itanisaidia kuwa mkufunzi wa maisha ya baadae na nashukuru Mungu sana kwa hilo.
Okwi alitawazwa kuwa mchezaji bora wa kigeni mara 2 katika ligi kuu ya soka akiwa kwenye club ya Simba, Tanzania Amesema ndoto zake ni kuwa Kocha ili asaidie vijana kucheza soka, ujuzi alionao ni mwingi. Amebaini kuwa ikiwa hilo halitowezekana anataraji siku za usoni kufanya kazi ya kusaka wachezaji wazuri kucheza kwenye vilabu vya soka.
Brightafrica.rw:
Kwenye ukanda huu ni wachezaji gani mashuhuri huwezi kuwasahau walipokuwa wakicheza mpira mpaka na wewe unafurahia kuwaona.

Emmanuel Okwi: Of course ukiangalia.. Fiston Mayele wa DRC , ukiangalia Haruna Niyonzima hapa Rwanda pia na huko Tanzania alikuwa maarufu sana, Afrika Mashariki nadhani wanamjuwa, wengine ni Chama wa Zambia, tulicheza naye katika timu ya Simba, yupo Meddy Kagere mnyarwanda mwenye asili ya Uganda na John Bocco wa Tanzania, ni wengi lakini hao siwezi kuwasahau.
Brightafrica.rw: Ni mchezaji gani wa kimataifa aliyekuvutia zaidi kumpenda wakati ukiwa mdogo?
Emmanuel Okwi: Ni mchezaji mmoja tu Thierry Henry wa Arsenal huyo nilimpenda sana kwa uchezaji wake nilipokwa mdogo. Wakati naanza kucheza nilivaa jezi Namba yake.
Bado nampenda huenda siku moja tutakutana huwezi kujuwa kwenye mambo yetu ya mpira. Na pia mimi ni mpenzi wa Arsenal.
Brightafrica.rw: Kwa kumalizia unapenda kula chakula gani?
Emmanuel Okwi: Napenda wali na maharage na ugali pia hapo najihisi vizuri.
Brightafrica.rw: Nashukuru kwa wakati wako.
Emmanuel Okwi: Asante
Christopher Karenzi
