BAL 2026: RSSB Tigers yaandika historia ya kutwaa taji la ubingwa
Christopher Karenzi
RSSB Tigers Basketball Club, imeandika historia jana Jumapili katika ukumbi wa BK Arena,jijini Kigali baada ya kuwa timu ya kwanza kutoka Rwanda na Afrika Mashariki kutwaa ubingwa wa Ligi ya mpira wa kikapu Afrika , Basketball Africa League (BAL) 2026dhidi ya mabingwa wa Angola Petro de Luanda kwa alama 90 kwa 88 katika mchezo huo wa fainali.
RSSB Tigers ilifanikiwa kuifunga Petro de Luanda ya Angola kwa alama 90 kwa 88 katika mchezo wa fainali uliokuwa wa kusisimua sana, ulioshuhudiwa pia na Rais wa Rwanda Paul Kagame.

Licha ya kuanza vibaya katika robo ya kwanza, RSSB Tigers ilionyesha moyo wa mapambano na kurejea kwa nguvu kubwa katika mchezo huo
Kocha mkuu wa RSSB Tigers BBC Henry Dennis Newton Mwinuka baada ya ushindi huu ameeleza kufurahia kwa kutwaa ubingwa ikiwa ni mara ya kwanza kutwaa taji hilo kwa mara ya kwanza. Amesema kwamba ni furaha isiyo na kifani kama Mtanzania, aliyepewa majukumu na Wizara ya Michezo na Shirisho la Basketball nchini Rwanda. Hii ni rekodi.
Nyota wa mchezo alikuwa Craig Randall II, ambaye aliongoza timu yake kwa kufunga alama 33, idadi kubwa zaidi katika fainali hiyo. Mchezaji huyo pia alitangazwa kuwa Mchezaji Bora wa Mashindano ya BAL 2026. Wakati huo huo, Muthiang Mangok alitunukiwa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ulinzi.

Mchezaji bora 2026 Nyota Craig Randall wa RSSB Tigers
Kocha wa Petro de Luanda, Sergio Valdeolmillos Moreno, alijaribu kufanya mabadiliko ya kimkakati katika dakika za mwisho kwa kumrejesha Gakou uwanjani ili kurejesha ushindani, lakini juhudi hizo hazikuweza kuizuia RSSB Tigers kutwaa ushindi.
Ushindi huu pia ni wa pili kwa RSSB Tigers dhidi ya mabingwa hao wa Angola katika msimu huu wa BAL, na unaiweka Rwanda katika historia ya mpira wa kikapu barani Afrika.Katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu wa BAL 2026, Al Ahly Benghazi ya Libya iliifunga Al Ahly ya Misri kwa alama 106–98

Kocha mkuu wa RSSB Tigers BBC Henry Dennis Newton Mwinuka
Kwa Craig Randall ushindi huu umehitimisha kampeni ya kipekee kabisa. Tayari alikuwa ameweka rekodi ya BAL kwa kufunga alama 54 katika mchezo mmoja, idadi kubwa zaidi kuwahi kufungwa katika historia ya mashindano hayo.
Katika fainali hii, aliendelea kung’ara na kuiongoza RSSB Tigers kutwaa taji lao la kwanza la Afrika mbele ya mashabiki wao wa nyumbani na familia yake, hususan mkewe Sarrah Marie.
Huu ni ushindi wa kihistoria usio na kifani kwa RSSB Tigers, kwa Rwanda, na kwa maendeleo ya mchezo wa mpira wa kikapu katika bara la Afrika.
Mchezo huo wa mwisho wa BAL 2026 ulifanyika tarehe 31 Mei 2026 na kuhudhuriwa na mashabiki 6,629 waliojazana ndani ya BK Arena. Rais wa Rwanda, Paul Kagame, alikuwa miongoni mwa waliohudhuria kushuhudia ushindi huo wa kihistoria.
Kocha wa Petro de Luanda, Sergio Moreno, na huzuni za kutotwaa ubingwa amesema: ‘’Hongera kwa Tigers kwa kutwaa ubingwa msimu huu. Hongera pia kwa wachezaji wangu. Ulikuwa mchezo mzuri sana, sana. Sina jambo lingine la kuongeza.”

Timu ya Petro de Luanda
Kwa msaada wa mashabiki waliokuwa wakishangilia kwa nguvu katika dakika nne za mwisho, Tigers ilifanikiwa kugeuza matokeo na kuongoza dhidi ya Petro de Luanda
RSSB Tigers waliingia kwenye mashindano hayo kupitia tiketi ya ARP BC, lakini kutokana na adhabu dhidi ya baadhi ya wakuu wa jeshi la nchi hii, APR haikushiriki. Hata hivyo, wachezaji wake walichanganywa na wale wa RSSB Tigers.
Katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu wa BAL 2026, Al Ahly Benghazi ya Libya iliifunga Al Ahly ya Misri kwa alama 106–98.
Michuano ya hatua ya Robo fainali, ilianza tarehe 22 Mei 2026 na kutamatika Jumapili. Huu ni ushindi wa kihistoria usio na kifani kwa RSSB Tigers, kwa Rwanda, na kwa maendeleo ya mchezo wa mpira wa kikapu katika bara la Afrika.

Mabingwa wa BAL 2026 RSSB Tigers
Michuano ya kwanza ilichezwa: 2021, Bingwa wa kwanza: Zamalek (Misri)
Bingwa wa 2026: RSSB Tigers BBC — timu ya kwanza ya Rwanda kutwaa taji hilo.
Tangu 2021 hadi 2026, BAL imefikia misimu sita, na Rwanda imekuwa mwenyeji muhimu wa hatua za mwisho za mashindano hayo
