Al Hilal SC Omdurman ya Sudan yashuka dimbani uwanja wa Pele kumenyana na AS Kigali
Na Christopher Karenzi
Dunia ya soka mashariki mwa Afrika inashuhudia sura mpya katika Ligi kuu ya Rwanda (Rwanda Premier League RPL), baada ya klabu mbili kongwe kutoka Sudan, Al Hilal SC Omdurman na Al Merrikh SC, kuthibitisha ushiriki wao rasmi na Shirikisho la soka la Rwanda FERWAFA katika ligi hiyo.
Timu ya Al Hilal SC Omdurman ina miadi na AS Kigali jumatatu hii katika Ligi Kuu ya Rwanda (Rwanda Premier League RPL),ikiwa ni mechi yake ya kwanza baada ya kuthibitishwa na Shirikisho la soka la Rwanda FERWAFA.
Rais wa timu hiyo, Yasir Hassan Ibrahim, amelishukuru shirikisho la FERWAFA kwa kuwapa fursa ya kushiriki kwenye ligi ya Rwanda, amesema .
‘’ Kwa niaba ya Bodi ya wakurugenz nashukuru Shirikisho la soka la FERWAFA kwa kutuunga mkono na kukubali ujio wetu wa kushriki ligi ya Rwanda. Hapa tunajisikia kama tuko nyumbani”.
‘’ Sisi tupo kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika (CAF Champions League), na tunaamini ligi hii itatusaidia katika maandalizi yetu. Ibrahimameongeza
Wakati huo huo, timu nyingine kutoka Sudan Al Merrikh SC tayari imewasili mjini Kigali, imeanza maandalizi ya kushiriki katika Ligi Kuu ya Rwanda. Kocha mkuu Darko Novic, kocha aliyewahi kuinoa APR FC, mabingwa watetezi wa ligi hiyo msimu uliopita alikuwa na haya ya.Kocha Darco amesema
Ligi ya Rwanda ni ngumu sana, si jambo rahisi kucheza hapa. Hakuna tofauti kucheza na timu ndogo au kubwa, kwa sababu kila timu inaweza kuishinda nyingine wakati wowote’’.
Al Merrikh itaanza mechi zake kwenye mzunguko wa 8 wa ligi, baada ya kukamilisha usajili na taratibu zote za Shirikisho la Soka la Rwanda (Ferwafa).
Kwenye michuano ya Ligi ya Klabu bingwa Afrika, Al Hilal SC kwenye Kundi C itacheza mechi zake za nyumbani mjini Kigali, itakapovaana na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, MC Alger ya Algeria, na FC Saint-Éloi Lupopo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Aidha , timu ya APR FC iliibwaga Rayon sports mabao 3-0 katika mchuano wa ‘’ Dabi ya Milima elfu moja’’ kwenye ligi kuu ya soka iliyopigwa kwenye uwanja wa Taifa wa Amahoro mwishoni mwa juma. Kocha mkuu wa Rayon Haruna Ferouz baada ya mechi hiyo amefanya mazungumzo na waandishi wa habari amesema kwamba magoli matatu kwenye derby ni mengi.Amebaini kuwa upungufu kwa timu yake ulikuwa katikati kwa wachezaji wa kiungo.

Mchezaji wa kiungo mshambuliaji Abed akitafuta mbinu za kuwaponyoka viungo wa APR
Kwa jumla timu ya jeshi la Polisi inaongoza kenye jedrwari la ligi katika mzunguko wa saba na alama 17, ikifuata Rayon sports na alama 12.
