Nsanzuwera Aandika Historia Kigali, atwaa Ubingwa wa SportsBiz Africa Golf
Na Christopher Karenzi
Mnyarwanda Celestin Nsanzuwera ameandika ukurasa mpya katika historia ya gofu barani Afrika baada ya kutwaa ubingwa wa SportsBiz Africa GolfChampionship iliyofanyika kwenye uwanja wa kimataifa wa Kigali Golf Resort & Villas ijumaa tarehe 5 Septemba 2025, ikiwa ni raundi ya tano ya Sunshine Development Tour – East Africa Swing. Shin
Mnyarwanda Celestin Nsanzuwera ametwaa ubingwa akicheza raundi ya mwisho kwa ustadi mkubwa na kutwaa ubingwa wa shindano la gofu maarufu ‘’SportsBiz Africa GolfChampionship’’ Akiwa chini ya matarajio makubwa ya nyumbani, Nsanzuwera alionesha utulivu na umakini, akifunga raundi ya mwisho kwa 2-under par 70, na kufikisha jumla ya 15-under par 201.
Raundi yake ilijumuisha birdies kwenye mashimo ya 1, 2, 8, 16 na 18, huku akikosea (bogeys) kwenye mashimo ya 2, 11 na 13.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kushindi, Nsanzuwera amesema:
“Ushindi huu una maana kubwa sana kwangu, hasa hapa nyumbani Kigali. Kulikuwa na shinikizo, lakini nilibaki makini kwenye mpango wangu na nikaamini maandalizi niliyofanya. Birdie kwenye shimo la 18 lilikuwa tukio la pekee, mbele ya mashabiki, na ilinipa fahari kubwa kubaki na ushindi nyumbani Rwanda’’. Nimecheza kila raundi ya Tour hii hadi sasa, na nahisi mchezo wangu unazidi kukua kila tukio. Ushindi huu unanipa kujiamini kuelekea raundi zijazo.”Kwa ushindi huo, Nsanzuwera alijinyakulia dola za Marekani 5,000 kati ya zawadi ya jumla ya dola 25,000.

Mshindi wa pili alikuwa Adam Breen kutoka Afrika Kusini, aliyetoa raundi bora kabisa bila kosa kwa 6-under par 66, na kufikisha jumla ya 10-under par 206.
Raundi yake ilihusisha birdies kwenye mashimo ya 1, 6, 8, 13, 17 na 18, na kumpa nafasi ya kipekee kama mmoja wa wachezaji waliovutia zaidi wiki hii. Breen amepokea kitita cha dola 2,675 kwa nafasi hiyo ya pili.
Breen amesema:
“Leo ilikuwa siku ambapo kila kitu kilienda sawa. Nilijipa nafasi nyingi na nikaweza kuzitumia hasa kwenye back nine ili kumuweka shinikizo kiongozi. Amecheza gofu ya hali ya juu wiki nzima na anastahili kabisa ushindi. Kwangu, kumaliza hivi kunanipa matumaini makubwa ya kujijenga kwa mashindano yajayo.”
Mshindi mara mbili wa DP World Tour na bingwa wa Kenya Open 2015, HaydnPorteous wa Afrika Kusini, alimaliza nafasi ya tatu kwa jumla ya 8-under par 208 baada ya raundi ya mwisho ya 2-under par 70. Alipata birdies kwenye shimo la 4, 7, 12 na 13, lakini akapoteza pointi kwenye shimo la 8, 14 na 15, kabla ya kumaliza kwa pars thabiti. Amezawadiwa dola 1,810.
Porteous alisema:
“Imekuwa ya kufurahisha sana kuwa hapa Kigali na kushuhudia ukuaji wa gofu Afrika Mashariki. Uwanja ulikuwa katika hali bora na ulikuwa mtihani wa kweli. Nimecheza vizuri, ingawa nimeacha nafasi chache. Lakini kuona wachezaji kutoka barani Afrika wakishindana kwa kiwango hiki ni jambo la kutia moyo. Nimeridhika na matokeo yangu na natazamia mashindano yajayo.”
Rais wa shirikisho la mchezo wa Gofu Balozi Bill Kayonga, baada ya shindano hili amefurahia sana ushiriki mkubwa katika maandalizi ya mashindano haya, hususan kwa namna ya pekee Mnyarwanda Celestin amenyakua ushindi leo kwa mara ya pili mfululizo katika mashindano yaliyohusisha mataifa mengi.

Kuhusiana na mchezo wa gofu nchini Rwanda, Balozi Kayonga amesema kwamba yapata takriban miaka 30 tangu kuanzishwa mchezo huo.
“Kutokana na nguvu zilizowekezwa katika mchezo huu, ndiyo sababu watu kama Celestin na mnyarwanda mwingine aliyefanikiwa kuwa miongoni mwa wachezaji 10 bora , pamoja na Byiringiro ambaye naye alicheza vyema katika mashindano haya.
Tunapopokea mashindano katika eneo hili mara nyingi tunamaliza katika nafasi ya 3, ilhali kuna mataifa mengine ambayo yamekuwa yakicheza gofu kwa muda mrefu zaidi.” Ameeleza Kayonga.
Kwenye shindano hili la siku tatu, nafasi ya nne ilinyakuliwa na Gaita Rodell wa Uganda na TravisProcter wa Afrika Kusini, wote wakiwa na jumla ya 7-under par 209, baada ya michezo mitatu mfululizo kwa siku tatu.
Mkenya Eric Ooko ndiye aliyeongoza miongoni mwa Wakenya, akichukua nafasi ya sita kwa jumla ya 6-under par 210. Wakenya wengine waliotamba ni Greg Snow na John Wangai, waliomaliza kwenye kumi bora kwa nafasi ya 8 kwa 4-under par 212.
Kwa upande wa amateurs wa juu, Wakenya Michael Karanga na John Lejirma walimaliza juu zaidi, wakifungana nafasi ya 12 kwa jumla ya 1-under par 215.
Mashindano ya SportsBiz Africa Golf Championship yaliwaleta kwa pamoja wachezaji 121 kutoka nchi 16 za Afrika, pamoja na washiriki kutoka Uingereza na Canada. Mashindano haya yalidhaminiwa na SportsBiz Africa, East African Breweries PLC kupitia chapa ya Johnnie Walker, Kigali Golf Resort & Villas, na Pure Travel.
Kama raundi ya tano ya Sunshine Development Tour – East Africa Swing, mashindano haya yalitoa sio tu zawadi ya dola 25,000, bali pia pointi muhimu za Sunshine Development TourOrder of Merit, pointi za Official World Golf Ranking (OWGR) na pointi za World Amateur Golf Ranking (WAGR).
