Wachezaji 60 Kutoka Nchi 21 Barani Afrika wakutana Kambini jijini Kigali

Share Now

Na Mwandishi wetu Christopher Karenzi

Kwa mara ya kwanza, katika Afrika ya Mashariki na Kati, Rwanda ni mwenyeji wa kambi ya mchezo wa mpira wa kikapu  maarufu Basketball Without Borders (BWB) inayokutanisha vijana 60 wenye umri wa miaka 18 na chini  kutoka katika nchi mbalimbali za Afrika.

Toleo la 21 la Basketball Without Borders (BWB) Afrika, lilianza rasmi kwenye viwanja vya ndani vya  Petit Stade na BK Arena, jijini Kigali, Rwanda jumamosi tarehe 23 Agosti 2025 likiwa na msisitizo mkubwa wa kuhimiza ushiriki wa wasichana katika mchezo wa mpira wa kikapu barani Afrika. Kambi imepangwa kumaliza shughuli zake Jumanne tarehe 26 Agosti 2025 kwenye viwanja vya ndani vya  Petit Stade na BK Arena, jijini Kigali, Rwanda.

Basketball Without Borders ni mpango ulioanzishwa kwa ushirikiano kati ya Ligi ya Mpira wa Kikapu Marekani (NBA) na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Kikapu (FIBA), ukiwaleta pamoja vijana wenye vipaji vinavyoahidi, kuwapatia mafunzo kutoka kwa makocha, wachezaji mashuhuri na nyota wa NBA pamoja na WNBA.

Washiriki hao wanajifunza mbinu na uzoefu kutoka kwa wachezaji wa sasa na wa zamani wa NBA na WNBA, pamoja na makocha mashuhuri.

Miongoni mwa viongozi na wakufunzi waliopo  ni pamoja na Clare Akamanzi, Mkurugenzi Mtendaji wa NBA Africa,Michael Finley, Mkuu wa NBA nchini Kenya Troy Justice, Mkuu wa Operesheni za Mpira wa Kikapu Kimataifa na Kita Matungulu, Mkurugenzi wa Operesheni za NBA Africa.

Kambi hii ya Basketball Without Borders inatarajiwa kutoa nafasi kwa vijana wa Kiafrika kukuza vipaji vyao na pia kujifunza nidhamu, uongozi na mshikamano kupitia mpira wa kikapu.

Miongoni mwa viongozi na wakufunzi waliopo  ni pamoja na Clare Akamanzi, Mkurugenzi Mtendaji wa NBA Africa,Michael Finley, Mkuu wa NBA nchini Kenya Troy Justice, Mkuu wa Operesheni za Mpira wa Kikapu Kimataifa na Kita Matungulu, Mkurugenzi wa Operesheni za NBA Africa.

Kambi hii ya Basketball Without Borders inatarajiwa kutoa nafasi kwa vijana wa Kiafrika kukuza vipaji vyao na pia kujifunza nidhamu, uongozi na mshikamano kupitia mpira wa kikapu.

Akizungumza katika mahojiano wakati wa uzinduzi wa kambi hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBA Afrika, Clare Akamanzi, alisema kuwa kambi ya BWB Afrika ni fursa ya kuwaonyesha wasichana vijana kuwa kuna nafasi kwao katika mchezo wa mpira wa kikapu. “Kwa sababu, ingawa michezo kwa ujumla imejaa wanaume, wasichana wengi zaidi sasa wanapata taaluma nzuri kupitia mpira wa kikapu na michezo kwa ujumla. Na programu kama BWB ni njia ya kuwaonyesha wasichana kwamba nao wanaweza kucheza mpira wa kikapu. Na wanaweza kucheza kwa mtindo wao wenyewe,” alisema.


Share Now

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *