WWF – APAC: Uzinduzi wa Mpango Mkakati wa Afrika 2021-2025
Kongamano kuhusu hifadhi ya mazingira jijini Kigali iliyofanyika kuanzia tarehe 18 lilitamatika tarehe 23 Julai 2022 iliwaleta kwa pamoja zaidi ya watu 2,500 kutoka nchi mbali mbali
Kwa wiki nzima washiriki wa mkutano walikuwa wakijadili uwakilishwaji na kuhakikisha uwepo wa wanajamii kwenye hifadhi ya mazingira haswa ukizingatia kwamba rasilimali za siri ziko kwenye jamii.
Kumezinduliwa ripoti ambayo inazungumzia jinsi pesa zilizotengwa kwa minajiri ya kuhifadhi, zinawafikia walengwa ambao ni mashirika yanayofanya uhifadhi barani Afrika
Jean Bakouma ni Mkurugenzi wa uhifadhi wa Bonde la Congo, akiwa na makao nchini Cameroon, akiongea na brightafrica.rw kuhusu kongamano hilo, amezungumzia juu ya maeneo ya uhifadhi katika bara la Afrika, amesema ‘’Tulichukua fursa hii kujadiliana kuhusu mkakati wetu wa Afrika juu ya uhifadhi wa maeneo yaliyohifadhiwa ya Afrika.
Utazingatia mambo muhimu ambayo ni muhimu, kuna mkakati unaohitaji mpangilio mzuri, ambao naweza kusema kwamba kuna utaratibu mzuri na utawala bora, utaratibu mwafaka na madhubuti wa kuchukua maamuzi’’.
Bakouma ameongeza kuwa jambo jingine ni taratibu wa utekelezaji wa kujenga kwa ushirikiano na wadau ili kuhakikisha ushirikishwaji wao katika hatua zitakazopelekea kuwa na uhalali.
Bakouma alisema kuhusu utelelezaji wa mpango huo ‘’mpango mkakati mpya wa WWF Afrika unatoa mfumo wa kuunganisha kazi ya Shirika katika kanda na kupata matokeo ili kuimarisha uhifadhi barani Afrika’’.
Hata hivyo kuna changamoto, ahadi hizi kutimizwa na mtu mmoja au shirika moja si rahisi.
Bwana Bakouma alisema inabidi wawe na sauti moja ‘’Ni lazima tushughulikie changamoto na fursa hizi pamoja kama nguvu zetu, mkusanyiko katika jamii, nchi, sekta na mitazamo ya sera inayokuja pamoja kama sauti moja.

Alice Ruhweza ni mkurugenzi wa kanda ya Afrika amefanya kazi na shirika hilo tangu julai 2019,
Ni miongoni mwa walioshiriki kongamano la hifadhi ya mazingira.
Jukumu lake ni kuendeleza na kuongoza Shirika la hifadhi la WWF barani Afrika ili iwe na ushawishi mkubwa na kuwa na ajenda barani Afrika.

Mara baada ya kutamatika kongamano hili, nilioongea pia na Philip Muruth, Makamu Mwenyekiti wa Shirika la uhifadhi wa mazingira na wanyama pori African Wildlife Foundation. Nilianza kumuuliza umuhimu wa mkutano huo.
Alisema nchi 53 zilishiriki na nchi 27 zilitoka mataifa mengine duniani zilishiriki kongamano lenyewe jijini Kigali, mkutano huo ulikuwa muhimu kwani ni mara ya kwanza kufanyika Africa parca Congres ilikuwa mara ya kwanza kukutana na kujadiliana tutahifadhi mazingira namna gani, kanini na kwa faida ya akna nani?
Miongoni mwa maazimio ya kongamano, waliazimia kuwa wanawake (Gender balance) na vijana, hao ndio viongozi wa sasa. Wamekubaliana pia kuhusu mabadiliko ya tabia nchi (Climate change)
Muruth amesema’’ Hii itatuathiri vibaya inabidi kupunguza makali juu ya mabadiliko ya tabia nchi, hizi sehemu za uhifadhi’’.
Kama mkenya alifurahia jiji la Kigali lilivopambwa na kupandwa miti sehemu ambazo ni za kimaumbile ndani ya mji.
Philip Muruth, amefanya katika Shirika la African Wildlife Foundation zaidi ya miaka 20.
Bara la Afrika lina takriban elfu nane na mia tano sehemu ya maeneo yaliyohifadhiwa huku takriban watu milioni miatatu wakitegemea hifadhi hizi kwa pato lao la kila siku.

Christopher Karenzi
