Mjini Kigali kunafanyika Kongamano la kimataifa la wiki moja kuhusu maeneo ya hifadhi barani Afrika
Kongamano hili limeanza tarehe 18 hadi Julai 23, 2022, limewaleta kwa pamoja watu zaidi ya elfu mbili mjini wakiwemo viongozi, wadau na wananchi kutoka mataifa mbali mbali wakijadili juu ya faida ya maeneo hifadhi katika kuhifadhi mazingira barani Afrika.
Nancy Githaiga ni mkurugenzi wa shirika la African Wildlife Foundation AWF likiwa na makao yake nchini Kenya, amesema kwamba ili kuziba pengo la maeneo ya hifadhi (protected areas), sehemu hizo ni zile za serikali na zile za watu binafsi ambazo husimamiwa na jamii.

Barani Afrika wanaongelea takriban elfu 8,600 sehemu ambazo zimehifadhiwa . Miongoni mwa hifadhi hizo ni mbuga ya wanyama ya Serengeti nchini Tanzania, mbuga ya wanyama ya Nairobi na Virunga upande wa Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda.
Bi Githaiga amesema ‘’ Wanyamapori na mchanga wetu ni rasilimali yetu waafrika hatuna maendeleo ya kiviwanda kwa hivo hii ndio rasilimali yetu’’.
Ili kufanikisha kuziba pengo upande wa sehemu za hifadhi, mkurugenzi Githahaiga amebaini kuwa dolla milioni 7 kwa mwaka zonahitajika kusaidia angalau kila mwaka zoezi hilo la hifadhi.
Ka upande wa Afrika ya mashariki Bi Gathaiga, ameongeza kuwa wanaafrika ya mashariki wangekuwa mbali zaidi, eti mambo muhimu wanayofanya yanabadilika.

Kongamano hili la kimataifa kuhusu maeneo ya hifadhi, limeandaliwa na IUCN Africa Protected Areas Congress pamoja na African Wildlife Foundation (AWF).
Christopher Karenzi
