Nchini Rwanda zipo timu 3 bora ambapo kila mmoja inapambana ili iweze kushiriki mashindano ya kimataifa ya mpira wa kikapu Basketball Africa League (BAL) .
Timu ya APR BBC ni mwakilishi wa Rwanda katika fainali za kombe la BAL, imefanya usajiri huku ikijiandaa mashindano ya mchujo ya BAL. Jumatano wiki hii ilipata chamtemakuni, ilifungwa na Patriots BBC kwa alama 73-59 ni dabi ya Kigali.
Kocha mkuu wa Patriots mtanzania Henry Mwinuka alifanya mahojiano na RFI Kiswahili-michezo. Aidha, aliifunga timu ya nishati REG wiki iliyopita na wiki hii amichapa APR. Kocha Mwinuka ametwaa vikombe 5 vya ligi katika timu mbili tofauti REG na Patriots katika uwanja wa LDK . Amesema asilimia 80 anatwaa ubingwa wa ligi msimu huu.
Hakuna kocha mwingine hapa nchini ambaye amethubutu kufanya kitendo kama hicho kwa timu mbili kabambe.
APR iko kwenye kundi moja na US Monastir mabingwa watetezi wa BAL 2022, AS Duanes yaSenegal pamoja na River Hoops ya Nigeria kuanza tarehe 4-12 Mei 2024.at STECOL.
Mechi hii ya kirafiki itasaidia APR kujiandaa mashindano ya mchujo kuelekea mechi za hatua ya Robo fainali ya Kombe la BAL.
Hayo yakiarifiwa, timu ya FUS Rabat kutoka Moroc na Petro de Luanda ya Angola tayari zimefuzu fainali kushiriki mashindano ya BAL jijini Kigali mei baada ya kushinda mechi zao nchini Afrika ya Kusini mwishoni mwa juma.
Timu hizo zilikuwa pamoja na Dynamo kutoka nchini Burundi lakini ilifurushwa kabla ya kucheza mechi yake ya pili wakiwa nchini Afrika ya Kusini. Kisa na mkasa walikataa kuvaa jezi zenye maandishi ya visit Rwanda.
Shirikisho la mpira wa kikapu nchini Burundi liliwakataza wasivae hizo jezi ambapo mdhamini mkuu ni Rwanda kupitia mradi wa Visit Rwanda.
Hii imepelekea kusimamishwa kwa timu hiyo kwa kipindi cha miaka mitano na kutozwa faini ya dola za kimarekani laki tano.


Christopher Karenzi
